Psalms 79:1-4

Maombi Kwa Ajili Ya Wokovu Wa Taifa

(Zaburi Ya Asafu)


1 aEe Mungu, mataifa yameuvamia urithi wako,
wamelinajisi Hekalu lako takatifu,
wameifanya Yerusalemu kuwa magofu.

2 bWametoa maiti za watumishi
kuwa chakula cha ndege wa angani
na nyama ya watakatifu wako
kwa wanyama wa nchi.

3 cWamemwaga damu kama maji
kuzunguka Yerusalemu yote,
wala hakuna yeyote wa kuwazika.

4 dTumekuwa kitu cha aibu kwa jirani zetu,
cha dharau na mzaha kwa wale wanaotuzunguka.

Copyright information for SwhKC